Mchezaji wa kimataifa wa Brazil Paulinho leo ametambulishwa na Tottenham baada ya kukimilisha uhamisho wa paundi millioni 17 Corinthians ya Brazil. Lakini wakati mchezaji huyo akitambulishwa mchezaji mwenzie wa timu hiyo beki wa kimataifa wa Cameroon
Assou-Ekotto ameiambia Goal.com: ' Simfahamu hata alivyo. Simjui, mie sifuatilii habari za namna hiyo. Mfano mzuri ni miaka mitatu iliyopita, Rafael van der Vaart alikuwa ndio amekuja mazoezini mara ya kwanza, nilimsalimia lakini sikuwa najua kama yeye ndio Rafael van der Vaart."
Comments
Post a Comment